Dar es 
Salaam. Wakati Bunge la Kujadili Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano
 wa Tanzania linaanza kikao chake kesho mjini Dodoma, wasomi na 
wanazuoni wapatao 300 wanakutana Dar es Salaam leo kujadili rasimu hiyo,
 mjadala mkuu ukilenga Muundo wa Serikali unaofaa nchini.
Mkurugenzi 
Mtendaji wa Taasisi ya Umoja wa Utafiti wa Programu za Vyuo Vikuu Kusini
 na Mashariki mwa Afrika (ESAURP), Profesa Teddy Malyamkono alisema Dar 
es Salaam jana kwamba kongamano hilo litajadili tafiti za wasomi hao 
ambazo zimekusanywa katika kitabu kimoja.
Alisema 
kitabu hicho ambacho kinajulikana kama Katiba Bora Tanzania, 
kinajumuisha mada mbalimbali ambazo zinalenga kuibua mjadala juu ya nani
 atakayenufaika na Muungano wa Serikali Tatu kama mapendekezo ya Rasimu 
itakayojadiliwa bungeni yanavyoeleza.
Pia 
kongamano hilo litajadili na kuchambua gharama za Serikali hizo na hasa 
maswali kama zitabebwa na nani? Zitasimamiwa na nani? Na vipi Zanzibar 
ambayo asilimia 90 ya wakazi wake ni Waislamu itamudu kujiepusha na 
masuala ya udini.
"Tunataka
 Muungano ambao utaendeleza mshikamano uliopo ndani ya nchi hivi sasa," 
alisema na kuongeza kuwa kuna vitu vingine vya kujadili iwapo Muungano 
utakuwa wa Serikali Tatu.... "Kama zitakuwa Serikali Tatu, nini hatima 
ya nchi hizo zilizoungana hususan katika uhusiano na mataifa mengine 
ambayo hayana ushirikiano na upande mmoja?"
Awali, 
akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Shule ya Sheria katika Chuo 
Kikuu Dar es Salam (UDSM), Profesa Boniventure Rutinwa alisema kuna mada
 ambayo itaakisi mapendekezo ya Kundi la G55 ambalo lilipendekeza mfumo 
wa Serikali Tatu lakini likapingwa bungeni. Profesa Boniventura pia 
aliikosoa Tume ya Warioba iliyokuwa ikikusanya maoni kuwa ilikuwa na 
walakini kwa kutokuwa na hadidu za rejea kama tume nyingine ikiwamo ile 
ya Jaji Robert Kisanga ambayo nayo pia ilikuwa na mapendekezo ya muundo 
wa Serikali Tatu.Dar es Salaam. Wakati Bunge la Kujadili Rasimu ya 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaanza kikao chake kesho 
mjini Dodoma, wasomi na wanazuoni wapatao 300 wanakutana Dar es Salaam 
leo kujadili rasimu hiyo, mjadala mkuu ukilenga Muundo wa Serikali 
unaofaa nchini.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Umoja wa Utafiti wa Programu za Vyuo Vikuu 
Kusini na Mashariki mwa Afrika (ESAURP), Profesa Teddy Malyamkono 
alisema Dar es Salaam jana kwamba kongamano hilo litajadili tafiti za 
wasomi hao ambazo zimekusanywa katika kitabu kimoja.
Alisema 
kitabu hicho ambacho kinajulikana kama Katiba Bora Tanzania, 
kinajumuisha mada mbalimbali ambazo zinalenga kuibua mjadala juu ya nani
 atakayenufaika na Muungano wa Serikali Tatu kama mapendekezo ya Rasimu 
itakayojadiliwa bungeni yanavyoeleza.
Pia 
kongamano hilo litajadili na kuchambua gharama za Serikali hizo na hasa 
maswali kama zitabebwa na nani? Zitasimamiwa na nani? Na vipi Zanzibar 
ambayo asilimia 90 ya wakazi wake ni Waislamu itamudu kujiepusha na 
masuala ya udini.
"Tunataka
 Muungano ambao utaendeleza mshikamano uliopo ndani ya nchi hivi sasa," 
alisema na kuongeza kuwa kuna vitu vingine vya kujadili iwapo Muungano 
utakuwa wa Serikali Tatu.... "Kama zitakuwa Serikali Tatu, nini hatima 
ya nchi hizo zilizoungana hususan katika uhusiano na mataifa mengine 
ambayo hayana ushirikiano na upande mmoja?"
Awali, 
akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Shule ya Sheria katika Chuo 
Kikuu Dar es Salam (UDSM), Profesa Boniventure Rutinwa alisema kuna mada
 ambayo itaakisi mapendekezo ya Kundi la G55 ambalo lilipendekeza mfumo 
wa Serikali Tatu lakini likapingwa bungeni. Profesa Boniventura pia 
aliikosoa Tume ya Warioba iliyokuwa ikikusanya maoni kuwa ilikuwa na 
walakini kwa kutokuwa na hadidu za rejea kama tume nyingine ikiwamo ile 
ya Jaji Robert Kisanga ambayo nayo pia ilikuwa na mapendekezo ya muundo 
wa Serikali Tatu.
CHANZO:MWANANCHI
0 comments :
Post a Comment