-->

JINSI MTAALA UNAVYOCHANGIA KURUDISHA NYUMA MAENDELEO YA ELIMU NCHINI TANZANIA

Assalaamu Alaykum. Hivi ulishawahi kutafakari kwa kina kwanini elimu tanzania inashuka kila wakati. Zipo sababu nyingi ila na mtaala unachangia kiasi fulani. Rejea mtaala wa sekondari (2007). Mwaka una siku (365), siku za mwanafunzi kuwa shule (194) tukitoa weekend (siku 138.57) ambazo ni sawasawa na majuma 19.79 ukilinganisha na majuma 52 kwa mwaka. Mwanafunzi anatakiwa kusoma vipindi visivyopungua 40 kwa wiki na kila kipindi kiwe na dakika 40. Hivyo mwanafunzi anasoma masaa 527.73 kwa mwaka ukilinganisha na jumla ya masaa 8760 ya mwaka.

Hitimisho kwenye mabano ndo hali halisi inayotakiwa kutendeka kwa mujibu wa data hizo hapo juu. mwaka 365 (138.57), miezi 12 (4.6), majuma 52(19.79), masaa 8760 (527.73) ambayo ni asilimia 6.02% ya maisha ya mwanafunzi kwa mwaka. Kwa hali hii unategemea nini? Chanzo NECTA tangu mwaka 2007 mpaka 2012 ni asilimia 14.33% waliofahuru kwa daraja la kwanza mpaka la tatu (yaani waliobatika kuendelea). Haya walimu kazi tunayo tufanyeje?
SOURCE:FB(NASHIR KAMUGISHA)
Share on Google Plus

About Unknown

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment