Uuzaji
 huo umetokana na ongezeko la maradhi ya figo miongoni mwa Watanzania 
kwani takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii zinaeleza kuwa kuna 
wagonjwa 470,000 nchini ambao figo zao zimeshindwa kufanya kazi kabisa 
na wanahitaji upandikizaji
 Katika
 kile kinachoonekana kukithiri kwa hali ngumu ya maisha, baadhi ya 
Watanzania wameanza biashara ya kuuza figo zao kwa gharama kubwa kwa 
watu wenye mahitaji ya kiungo hicho muhimu mwilini.
Uuzaji
 huo umetokana na ongezeko la maradhi ya figo miongoni mwa Watanzania 
kwani takwimu za Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii zinaeleza kuwa kuna 
wagonjwa 470,000 nchini ambao figo zao zimeshindwa kufanya kazi kabisa 
na wanahitaji upandikizaji. Katika uchunguzi wake, mwandishi wa gazeti 
hili alifanya kazi ya kutafuta kama wafanyavyo watu wengine wenye 
mahitaji hayo na alifanikiwa kukutana na watu kadhaa ambao walikuwa 
tayari kumwuzia lakini kwa gharama kubwa.
Kijana
 mmoja alikuwa tayari kumwuzia figo mwandishi wetu. Katika kufikia 
makubaliano mazungumzo ya kijana huyo, Abiyudi Mtaki na mwandishi wetu 
yalikuwa hivi:
Mwandishi: “Habari
 yako kaka, nimepata namba yako kutoka kwa (jina linahifadhiwa) amesema 
upo tayari kuuza figo yako, mimi nina shida kwa sababu mama yangu 
anahitaji na hali yake si nzuri.”
Muuzaji: “Nitumie meseji nipo kwenye gari.”
Alipotumiwa
 meseji alijibu hivi: “Dada yangu mimi naelekea Uganda, kuna mtu 
kanitumia tiketi jana, wakala nilimwambia kuwa nauza, ila yeye 
hakuniambia iwapo kuna mtu wa Dar es Salaam anayehitaji.”
Mwandishi: “Jamani kaka tusaidie kwa sababu tuna shida, kwani huyo wa Uganda anakupa shilingi ngapi?”
Muuzaji: “Napata milioni 80 aisee!”
Mwandishi: “Basi sitaweza kupata hizo fedha, ngoja niangalie namna nyingine.”
Muuzaji: “Kwani we ulikuwa na ngapi?”
Mwandishi: “Tuna shilingi milioni 20 tu.”
Kiwango hicho hakikukubaliwa na muuzaji huyo.
-MWANANCHI
0 comments :
Post a Comment