Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa 
Arusha, Liberatus Sabas, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea majira 
ya saa 3:45 usiku maeneo ya msitiki huo.
Hata hivyo, Kamanda alisema upelelezi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea ikiwa ni pamoja na kutumia kopo lililokuwa na kimiminika hicho ambacho kimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kujua uhalisia wake.
Hata hivyo, Kamanda alisema upelelezi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea ikiwa ni pamoja na kutumia kopo lililokuwa na kimiminika hicho ambacho kimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kujua uhalisia wake.
Akifafanua zaidi, Kamanda Sabas 
alisema, uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kwamba muda si mrefu 
kabla ya tukio hilo, Hassan, alikuwa anatokea maeneo ya kituo kikuu cha 
mabasi cha Arusha baada ya kuachana na wenzake wawili ambao walikuwa 
wanajadili kikao cha Maulid.
Alisema muda huo wa saa 3:45 
alikuwa maeneo ya karibu na kwake Unga Ltd, ndipo alipomuona mtu 
amesimama kwenye kiambaza cha msikiti, alimsalimia lakini hakumbuki kama
 alijibiwa.
Alisema wakati akiendelea kuelekea
 kwake, alihisi kuna mtu anamfuata na alipogeuka ili ajue ni nani, 
ghafla mtu huyo alimwagia kimiminika kinachosadikiwa kuwa ni tindikali.
Alisema mara baada ya kitendo hicho mtuhumiwa alikimbia na kuelekea kusikojulikana.
Alisema baada ya taarifa hiyo 
polisi waliokuwa doria maeneo ya karibu walikwenda katika eneo hilo na 
kukuta kopo dogo ambalo linasadikiwa kuwa lilikuwa na kimiminika 
kinachosaidikiwa kuwa na tindikali.
CHANZO:FULLSHANGWE 
 
0 comments :
Post a Comment