-->

MAPAPA WA UJANGILI 40 WAPATIKANA NA MTANDAO WAO WAFAHAMIKA HUKO ARUSHA


“Kuna majangili 40 waliotambuliwa na tumetambua mtandao mzima, pale Arusha kuna mtu mkubwa alikuwa anaendesha biashara. Kazi ilikuwa ni kutambua mtandano wote, ule mtandao ni mpana sana,” alisema Rais Kikwete
Rais Kikwete alisema: 

“Wakati wa uhuru Tanzania ilikuwa na tembo 350,000… Mwaka 1987 walibaki 55,000…Juhudi za kupambana na ujangili zimeanza muda mrefu. Tangu mwaka 1989 kulikuwa na Operesheni Uhai na tulifanikiwa, kwani mwaka 2009 idadi ya tembo ilifikia 110,000,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Mwaka 2010 kulizuka aina nyingine ya ujangili na hii ni ya upuuzi kabisa. Kwa mfano katika pori moja kulikuwa na tembo 30,000 na wote walikwisha… Ni jambo gumu sana.”

“Nchi zilizoendelea kama Uingereza na Marekani watatusaidia katika mafunzo na vifaa, silaha, uangalizi na vyovyote vile watakavyojitolea.”
Share on Google Plus

About Omari Makoo

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment