KUSTAAFU SIR ALEX FERGUSON: NINI WANASEMA??
Jumatano, 08 Mei 2013 16:58
>>CRISTIANO RONALDO: “ASANTE SANA KWA KILA KITU, BOSI!”
>>SEPP BLATTER: “NI NGULI!”
>>PAUL INCE: “HATUWEZI TENA KUONA MTU AINA HII!”
>>CHELSEA: “KILA LA HERI SIR ALEX FERGUSON! ALIKUWA MPINZANI SAFI KWA MIAKA 26!”
WADAU WENGI WALIIBUKA NA KUTOA MAONI YAO KAMA IFUATAVYO:
-Michael Owen, Mchezaji wa zamani wa Man United na England: “Ukisoma rekodi yake ya Umeneja utashtuka!”
-Mchezaji wa zamani wa Man United, Paddy Crerand: “Mungu amsaidie Mtu atakaemrithi kwani viwango alivyoviweka ni vya juu mno!”
-Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron: “Ni Mtu wa ajabu! Natumai kustaafu kwake kutaisaidia Timu yangu [Aston Villa]!!”
-Rais wa UEFA, Michel Platini: “Yeye ni
Mtu mwenye kuona mbali. Ametoa mchango mkubwa kwa Soka, si Scotland na
England tu, bali Ulaya yote na mbali kote.”
-Mkurugenzi Mtendaji wa Man United,
David Gill: “Alichoifanyia Klabu hii na kwa Soka kwa ujumla
hakutasahauliwa milele. Nimepata mafunzo mengi kwa kufanya nae kazi na
ni heshima kubwa kwangu kumuita ni Rafiki yangu.”
-Nahodha wa zamani wa England na
Mchezaji wa Man United, Paul Ince: “Hutaweza tena kumuona Mtu wa aina
hii tena. Viwango vyake vilikuwa vya juu. Alikuwa akitaka Watu wajitume.
Ndio, tulikuwa na migongano yetu. Lakini alinichukulia mimi kama
Mwanawe. ”
-Kiungo wa zamani wa Man United, Lou Macari: “Je huyo anaekuja kumrithi anaweza kufanya alichofanya Sir Alex? Ni ngumu!”
-Mchezaji wa Real Madrid aliewahi kuwa Man United, Cristiano Ronaldo: “Asante sana kwa kila kitu, Bosi!”
-Rio Ferdinand, Beki wa Man United: “Bosi anatetea kila Mchezaji kwa kila kitu na ndio maana Wacheza wote wanamuheshimu sana!”
-Nayo Klabu ya Chelsea ilituma Ujumbe
kwenye Twitter: “Wote hapa Chelsea tunamtakia kila la heri Sir Alex
Ferguson kwa kustaafu. Alikuwa Mpinzani safi kwa Miaka 26!”
-Kipa wa zamani wa Man United, Peter
Schmeichel : “Hili limekuja kama Bomu. Nimehuzunika na kuvunjwa moyo.
Nilitegemea atakuwepo kwa Miaka kadhaa!!”
-Meneja wa Celtic, Neil Lennon: “Gemu haitakuwa kama ilivyokuwa bila Sir Alex Ferguson!”
credit to sokainbongo
0 comments :
Post a Comment