![]() |
Edelphonce Bilohe ‘Mkulima’ |
Pamoja na kutoelewa mchakato wa uteuzi huo, Bilohe alilalamika kuwa
tangu amefika Dodoma hajapata mapokezi mazuri kutoka kwa wana CCM
wenzake au hata wale watia nia 38 waliobahatika kurudisha fomu.
“Kila ninapojaribu kuuliza hiki au kile sipewi majibu, nimekaa hapa na wanaCCM wa mkoani, sijaonana na Nape (Nnauye) wala (Abdulrahman) Kinana, wala watia nia wenzangu”
Alisema anashangaa kuwa hajahojiwa kama utaratibu wa uteuzi huo unavyotakiwa badala yake ameshindwa hata kujua wanaCCM wenzake walipo na wanafanya nini kwa wakati huo.
“Kuna makundi hapa, hali si nzuri, mpaka sasa sijaelezwa utaratibu wa mkutano wa halmashauri unavyokwenda. Nimezunguka nchi nzima, nitawaambia nini Watanzania. Hali ya hapa imeharibika”
Bilohe alisema hajaridhishwa na mchakato wa kumpata mgombea na alieleza
kufurahishwa kwake na hatua ya Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Dk Emmanuel
Nchimbi, Sophia Simba na Adam Kimbisa kuyapinga.
0 comments :
Post a Comment