Mkuu wa
shirika la Umoja wa Mataifa la kuwashughulikia wakimbizi UNHCR, Antonio
Guterres ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwamba, hatua
za haraka zisipochukuliwa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Waislamu wa nchi
hiyo watauawa wote.
Mkuu huyo
wa UNHCR ameongeza kuwa, kundi la Kikristo la Anti-Balaka limehamia
magharibi mwa CAR wanakoishi Waislamu wengi na kwamba yumkini wakafanya
mauaji ya kutisha dhidi ya Waislamu hao.
Hii ni
katika hali ambayo, Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya mpito ya
Jamhuri ya Afrika ya Kati, Toussaint Kongo-Doudou, ameliomba Baraza la
Usalama la UN liidhinishe kupelekwa wanajeshi zaidi nchini humo ili
kudhibiti hali ya mambo.
Kongo-Doudou
amesema mauaji dhidi ya Waislamu yakiendelea itafika mahali nchi
itasambaratika na itakuwa vigumu kudhibiti hali ya mambo.
0 comments :
Post a Comment