-->

ZANTEL WATOA MAFUNZO MAALUMU KWA WAKAZI WA ZANZIBAR KUHUSU Z-KILIMO

Kampuni ya Zantel kwa kushirikiana na Umoja wa wakulima na matunda Zanzibar (UWAMWIMA), imetoa mafunzo kwa maofisa ugani 50 hapa Zanzibar ili kuwawezesha kutumia huduma ya Z-Kilmo ya Zantel. Huduma ya Z-Kilimo ya Zantel, inawawezewa wakulima nchini Tanzania kupata taarifa za papo kwa papo na uhakika kuhusu njia za kuendesha kilimo cha kisasa kwenye simu zao za mikononi.

Mkurugenzi wa Zantel Zanzibar, Mohamed Mussa 'Baucha' akifungua mafunzo kwa wakulima wa mbogamboga na ufugaji, mradi wa Z-KILIMO katika kuwasaidia wateja wa Zantel.

Ofisa Biashara Mwandamizi wa Zantel, Ibrahim Attas akitoa maelekezo ya matumizi ya simu kwenye mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Zantel kwa wakulima wa mbogamboga na wafugaji jana.
 
Ofisa Biashara Mwandamizi wa Zantel, Ibrahim Attas akitoa mafunzo kwa wakulima wa mbogamboga na wafugaji jana.Ofisa wa Zantel (kushoto) akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo, wakulima wa mbogamboga na wafugaji wa Zanzibar wakati wa mafunzo yaliyotolewa na Zantel kwenye ofisi zake Amani mjini Zanzibar jana
Share on Google Plus

About Omari Makoo

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment