Watu
watatu wafariki dunia mkoani Iringa katika matukio manne tofauti likiwemo la
Ponsian Vakuka (37) mkulima wa Ihowanza kufariki dunia baada ya kukatwa na
jembe kichwani.
Akizungumza
na mtandao huu wa www.matukiodaima.com
ofisini kwake leo Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi
alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 27 january majira
ya saa 1:30 jioni.
Mungi
alisema kuwa marehemu alifanyiwa kitendo hicho cha kikatili na mke wake aitwaye
Mwamvita Tinda (35) ambapo chanzo kilisemekana mwanamke huyo alikuwa amelewa
wakati akifanya mauaji hayo, hata hivyo mtuhumiwa amekamatwa.
Wakati
huohuo watu wawili wakazi wa Lulanda kata ya Ihanu tarafa ya Ifwagi wilaya ya
Mufindi waliuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za kishirikina.
Mungi
alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 2 februari majira ya saa 6 kamili
mchana ambapo aliwataja watu hao ni Alutal Kihongole (95) pamoja na Boscow Masonda (85) wote ni wakulima, hakuna
mtu aliyekamatwa kuhusiana na mauaji hayo.
Wakati
huohuo Elias Ngope (78) mkazi wa Kisonga tarafa ya Pawaga alikutwa akiwa
amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye bwawa la maji akiwa anaoga, chanzo
cha tukio hilo ni marehemu alikuwa anaugua ugonjwa wa kifafa.
Mbali
na matukio hayo ya kusikitisha, Kamanda Mungi alisema watu wasiofahamika
waliiba pikipiki yenye namba za usajili T. 507 CBE aina ya Sky mark ya rangi
nyeusi yenye thamani ya shilingi 1,800,000/= mali ya Simaitoni Kionza (33)
mkazi wa Ipogoro, ambapo watuhumiwa wanatafutwa.
SOURCE:DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA.
0 comments :
Post a Comment