
Inadaiwa kwamba raia wa China walitumia ziara ya rais wao nchini humo kusafirisha kimagendo maelfu ya kilo za pembe za ndovu.
Kulingana na shirika la utafiti wa mazingira, EIA, Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja tu kabla ya ziara ya rais huyo nchini tanzania mwaka jana na zilifichwa katika mifuko ya wanadiplomasia ili zisitambuliwe.
Msemaji wa serikali Assah Mwambene amemwambia mwandishi wa BBC Aboubakar famau kwamba ripoti kama hiyo zinatatiza jitihada za serikali kukabiliana na uuzaji haramu wa pembe za ndovu.
SOURCE:BBC SWAHILI
0 comments :
Post a Comment